Wapendwa wangu nachukua nafasi hii kuwashukuru wote ambao kila siku mmekua mkitenga muda wenu na kupitia blog yangu.
Sio kwamba hamna cha kufanya au hakuna cha kuangalia bali mnathamini mchango wangu katika kuhabarishana,kufundishana na wakati mwingine kuburudishana,NASEMA ASANTE SANA.
Ili kuboresha blog hii naomba mnisaidie mawazo nini kifanyike ambacho mngependa kiwe kinawekwa humu? Nitafurahi sana kupata mapendekezo yenu zaidi kwani kuna walioomba post nyingi ziwe kwa Kiswahili badala ya kingereza hilo nimelipokea lakini ningependa kujua zaidi kutoka kwenu wapendwa.
Natanguliza shukrani za dhati kabisa.
Nawatakia siku njema na utendaji mzuri wa kazi.
Majoy.
No comments:
Post a Comment
Thank you for your comment