Social Icons

Wednesday, March 6, 2013

TASWIRA ZA ABSALOM KIBANDA AKIWA HOSPITALINI MUHIMBILI BAADA YA KUVAMIWA NA KUUMIZWA VIBAYA


Waziri wa Afya, Dk. Hussein Mwinyi, akimjulia hali Absalom Kibanda katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Magazeti ya Habari Corporation, Hussein Bashe, akimpa pole Kibanda.…


Waziri wa Afya, Dk. Hussein Mwinyi, akimjulia hali Absalom Kibanda katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Magazeti ya Habari Corporation, Hussein Bashe, akimpa pole Kibanda.

Kibanda akiwa wodi ya wagonjwa mahututi (ICU).

 Wanahabari wakimjulia hali Kibanda pamoja na kupata machache kutoka kwake. 

Kibanda akiendelea kupata matibabu ICU.

Dk. Reginald Mengi (kushoto) akibadilishana mawazo na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova.   

Waziri wa Afya Dk. Hussein Mwinyi akibadilishana mawazo na Prof. Lawrence Maseru wa MOI.

Mwenyekiti wa makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi (kulia) akimpa pole, Afisa Mtendaji Mkuu wa Magazeti ya Habari Corporation, Hussein Bashe.
Baadhi ya majeraha aliyoyapata Kibanda.

MWENYEKITI wa Jukwaa la Wahariri na Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Habari Corporation, Absalom Kibanda, usiku wa kuamkia leo amevamiwa na watu wasiojulikana wakati akivuka geti kuingia nyumbani kwake na gari yake aina ya Nissan. 
Wavamizi hao walivunja kioo cha gari lake na kumchomoa ambapo walimpiga mapanga na kumjeruhi vibaya jicho la kushoto. Baada ya kufanyiwa unyama huo Kibanda alikimbizwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kupatiwa matibabu ambapo amelazwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi ‘ICU’.


(PICHA ZOTE : RICHARD BUKOS NA HARUNI SANCHAWA / GPL)

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS.


No comments:

Post a Comment

Thank you for your comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...