Monday, April 30, 2012
TUWASAIDIE JAMANI KILA MTU KWA KADRI UTAKAVYOBARIKIWA....
![]() |
| Juma Kilowoko (Sajuki) akiwa na mkewe Wastara siku walipofunga ndoa |
![]() |
| Wastara |
| Sajuki alivyo sasa baada ya kuugua |
Ndugu zangu Watanzania popote mlipo ulimwenguni tunaombwa kuisaidia familia hii kwa hali na mali kwa jinsi Mungu atakavyotubariki ili waweze kujikimu na maisha yao ya kila siku ikiwa ni pamoja na kupata pesa za matibabu ya Sajuki yanayotarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi milioni 25 za kitanzania.
Kama utaguswa kwa namna yoyote ile unaombwa kutuma mchango wako kupia akauti ya benki ya Wastara au kwa m-pesa kwa namba nitakazozitaja hapa chini.
AKIBA COMMERCIAL BANK, ACC NO. 050000003047, WASTARA JUMA
AU
KWA M-PESA NO. 0762 189592
Asanteni sana kwa ushirikiano wenu Mungu awabariki na azidishe kila mtakapopunguza.
(picha shukrani kwa Global Publisher)
Majoy.
Tuesday, April 3, 2012
DIVORCE ring!!!!!!
According to the jeweller, the idea is for women to buy the ring for themselves at the end of their marriage and wear it on their wedding finger as a defiant ''(I Don't!)''
![]() |
| Divorce ring |
The DIVORCE ring is 18 ct goldplated electroformed bird skull with swarovski crystals. Due to the electroforming technique, each piece is unique.
''Mourning is not just about dead people, it is also about dead relationships and decaying marriages. Today, 42% of the marriages finish by divorce in UK and 38% in France. My divorce jewellery refers to old and contemporary wedding customs to illustrate this sort of mourning. As a French, most of these customs come from France as the Bride Globe which it is a present to the bride to put her bouquet and her crown after the wedding. All the decoration inside symbolize the union and give luck to the marriage. I use union and marriage symbols and subvert them to show the inevitability of the breakup, but also show that from these ashes may raise a new life'' Said Gisele Ganne(A french jeweller)
For more description of the devorce ring visit here
Monday, April 2, 2012
CHADEMA OYEEEEEEE!!!!
Matokeo ya kura za Ubunge jimbo la Arumeru Mashariki yametangazwa sasa hivi na Msimamizi wa Uchaguzi na Mkurugenzi wa Wilaya ya Arumeru Bw Gracias Kagenzi amemtangaza mgombea wa CHADEMA Bw Joshua Nassari kuwa mshindi baada ya kupata kura 32,972 dhidi ya mpinzani wake wa karibu kutoka CCM Bw Sioi Sumari aliyepata kura 26,757
Matokeo kwa Vyama vingine sita vilivyoshiriki ni kama ifuatavyo:-
DP -77
NRA – 35
AFP – 139
UPDB – 18
TLP – 18
SAU – 22
Kwa mujibu wa Bw Kagenzi zaidi ya watu 120,000 walijiandikisha na aliojitokeza na kupiga kura walikuwa 60,696 ambapo kura halali zilikuwa 60,038 na zilizoharibika ni kura 661.
Wakati huo huo, habari kutoka Mwanza zinasema CHADEMA kimeshinda katika uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kirumba mkoani Mwanza.
Msimamizi wa uchaguzi huo, Bw. Aloyce Mkono, amemtangaza kuwa mshindi mgombea wa Chadema Mh Dany Kahungu kwa kura 2,938 dhidi ya mgombea wa CCM Mh Jackson Masamaki aaliyepata kura 2,131.
Wagombea wengine walioshindwa vibaya katika uchaguzi ni pamoja na Mh Haji Issa wa CUF aliyepata kura 184, Mh Kasala Muhana wa UDP amepata kura 7 na Mh Athuman Jumanne wa NCCR Mageuzi aliyeambulia 0 katika uchaguzi huo .
Msimamizi huyo alisema kuwa uchaguzi huo umefanyika katika hali ya amani na utulivu,na kuwashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi huo na kuonyesha utulivu mkubwa wakati wa uchaguzi na zoezi la kutangazwa kwa matokeo.
Habari na Picha, Shukrani kwa Mo Blog
Subscribe to:
Posts (Atom)







